Fid Q feat Barakah The Prince - MAFANIKIO ( OFFICIAL LYRIC VIDEO )

  • intro: Barakah The Prince
    kila mtu anataka mafanikio..
    verse 1:Fid Q
    Kujisikia nipo juu mie sitaki hizo deals/
    sipendi makuu hivyo nitabaki kuwa real../
    na kila track ya Q aaah,.. ni wazi utaifeel/
    ni wazi iko full aah MZAZI ninakill/
    ninamwagika kama Masika../ ninaheshimika na sio kanjibai/
    kwa huu mziki wa bajaji hadi kwa washkaji wenye macadillac/
    unawashika ile kibabylon.. unauzika sana maghetoni/
    ilimradi tu wawe happy more..midadi tu ila party noooo/
    mkisinzia mtaniudhi nishawapa vyeo/
    tuwape wapuuzi waliodai hii haiuzi haya matokeo/
    safari ni hatua.. kufika inabidi uianze/
    haina kukita au kusita.. inabidi ukaze/
    ingia, ongoza au fuata mkia, kukimbia ni mwiko/
    kuanzia ulipo sio sawa na kubakia ulipo/
    nikisema 'chini hapana' nina maana fanya unyanyuke/
    na ukiamini umesimama mwana.. komaa usianguke/
    ukijituma na neema inakaribia../
    nyuma walio-give up mapema wangekaza wangeifikia/
    penye... happy.. jitusu.. unafki usiuruhusu/
    yajue ya kuzingatia ili uachane na yasiyokuhusu/
    kibongobongo longolongo shazi/
    endelea kusaka mchongo hata ukipata kazi/
    HOOK: Barakah the prince
    Tunachukiana? ndio../
    ila sio sababu kuacha riadha ya mafanikio/
    ongeza mbio/
    sababu kila mtu, kila kona anasaka mafanikio/
    haukungoji wakati.. ooh wewe/
    zinapita nyakati..ooh wewe/
    muda wako bahati.. oh wewe/
    verse 2:Fid Q
    Na kughairisha kisa haupati sapoti/
    ni kujificha na kuuliza giza.. iko wapi ile tochi?/
    haupati ile noti/
    na wakati wa ule uboss ushapotea/
    hautaki ukose? usiache ofcoz endelea/
    utafanikiwa kwa unachojua au unachofanya/
    wachache ndio hutusua kwa jinsi tu wanavyoonekana/
    mafanikio hayaji ukikata tamaa../
    yenyewe huwafuata wanaojituma na wale wasiosukumwa na njaa/
    sipigi kila dili mipaka imezingatiwa/
    sitaki kuwa tajiri ninataka kufanikiwa/
    ili kuheshimiwa kwanza ni lazima ujiheshimu/
    lakini kufanikiwa ni maujanja tu sio lazima elimu/
    ili kuyadaka wengine hugeuka wabaya/
    mafanikio kwenye kuyasaka wengine hugeuka malaya/
    hugeuka was(i)o haya/
    kutwa utawakuta kwa babu/
    na anayefanya mambo ya maana huwa hana muda wa kuyahesabu/
    kwenye kuyasaka hakikisha haufilisiki/
    haupotezi maisha au vile vitu havinunuliki/
    sio kama hatucheki kwasababu tumezeeka?/
    nope.. ni tunazeeka kwasababu hatujawahi cheka/
    HOOK: Barakah the prince
    Tunachukiana? ndio../
    ila sio sababu kuacha riadha ya mafanikio/
    ongeza mbio/
    sababu kila mtu, kila kona anasaka mafanikio/
    haukungoji wakati.. ooh wewe/
    zinapita nyakati..ooh wewe/
    muda wako bahati.. oh wewe/
    utumie basi... eeeh eeeh/
    bridge: Barakah The Prince
    una mpenzi (na) uko lonely?/
    im sorry ndugu.. haujafanikiwa/
    maisha ni kama boli, magoli ndio kufanikiwa/
    oooh ooh oooh..oooh.. ndio kufanikiwa/
    kila mtu anataka mafanikio.../
    outro:Barakah The Prince
    hhhmmm.. hhhhmmm.. oh mafanikio
    oh mafanikio
    kila mtu anataka mafanikio

    Category : Tanzania Music Videos

    #fid#q#feat#barakah#the#prince#mafanikio#official#lyric#video

    0 Comments and 0 replies
arrow_drop_up